08/01/2026
Kiswahili
Tuzungumze Michezo
08/01/2026
Kiswahili
Kubeti Kunahitaji Akili Timamu
21/10/2024
SHABIKI wa Yanga unayeshangilia ushindi wa timu yako soma hii, namna mabosi wa klabu yako na kipa wenu Djigui Diarra alivyosafirishwa kimafia kuiwahi mechi dhidi ya Simba, akishuka Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal 3 na kufika uwanjani kisha akaibeba timu yako.
Kipa huyo juzi alitua uwanja wa ndege Dar es Salaam saa 8 mchana, kisha kwenda moja kwa moja Uwanja wa Benjamin Mkapa akiisubiri timu yake na kikosi kilipowasili saa 9 alasiri akaungana nacho na kufanya kazi ya kishujaa.
Iko hivi; Oktoba 15 Mali ilikuwa ugenini Guinea Bissau ikicheza mechi ya kuwania nafasi ya kushiriki Fainali za Kombe la Mataifa Afrika, mechi iliyoisha kwa suluhu huku kipa huyo akiwa golini.
Baada ya mchezo huo, alilazimika kusubiri ndege maalum ya kuwarudisha Mali lakini baadaye ikachelewa huku kukiwa hakuna ndege nyingine kwa haraka.
Kipa huyo aliijulisha klabu yake haraka na msako wa kumleta nchini ukaanza na kupata nafasi moja pekee kwenye ndege inayotoka Guinea kwenda Senegal umbali wa kilometa 308 akitumia dakika 35 kufika.
Yanga ililazimika kumpeleka Senegal ikiwa ni taifa karibu na Guinea Bissau ambako angepanda ndege ya haraka ya kuunganisha
Hapo Senegal akapata ndege Oktoba 18 iliyompeleka hadi Dubai akisafiri umbali wa kilo meta 7640.04 alaunganisha ya kumleta Dar es Salaam.
Diarra k**a angechelewa kwa saa moja tu kufika Dubai, safari yake ingekwamia hapo kuwahi mechi ya Simba ambako alikuta tayari kuna maafisa wanamsubiri kumuwahisha kwenye ndege inayokuja nchini.
Kipa huyo akatumia saa 5:30 kusafiri kutoka Dubai hadi Dar es Salaam umbali wa kilometa 3999.23 akiwasili saa 8:00 mchana ambako nako alikuta watu wanamsubiri kuanzia ndani mpaka nje kumuwahisha uwanjani.
Diarra alitoka uwanjani hapo saa 8:20 mchana kisha kuwahishwa Uwanja wa Benjamin Mkapa akikuta hata wenzake hawajafika kutokea AVIC Town.
Mara baada ya kufika uwanjani, kipa huyo aliingizwa vyumbani na kuanza kutengenezwa kisaikolojia na mabosi wa Yanga kisha akawaambia yuko tayari kucheza mechi hiyo.
Ndani ya mchezo huo, Diarra hakuonyesha k**a ni kipa aliyekaribia kuukosa mchezo huo na dakika tano tu, akafanya kazi ya kibabe akiokoa majaribio mawili makubwa ya Simba
19/10/2024
Tuna Viongozi katika mpira wetu ambao wanaamini mchezaji hapaswi kukosea hata kidogo. YAANI kwao hawaaamini kabisa k**a kuna makosa kwenye football ...
Wanaamini kuwa mchezaji akikosea tu kanunuliwa. Mpira wa nchi hii una shida sana na Hii inaanzia kwenye Kuwa na Matarajio makubwa kuliko Uwezo
Juzi tu Stars kafungwa tukaanza kusema wachezaji hawajitumi ๐๐๐YAANI hatujitumi kwa CONGO DR ....
Ndo haya haya ya leo ....YES CAMARA kafanya makosa yameigharimu timu lakin Kiongozi Mkubwa anaolaumu mchezaji Public ๐๐๐dddek Wachezaji wetu wataendelea kudharaulika ๐๐.
MUWE NA SIKU NJEMA ๐๐๐UBAYA UBWELA
19/10/2024
Balaa
Ungekuwa wewe ni CAMARA ungejiteteaje kwa Boss wako na Boss ndio amewaka namna hii? Embu vaa uhusika wa Camara alafu jitetee kwaBoss.