Mbogella sport

Mbogella sport

Share

Habari za michezo ya aina zote na breaking news ndani na nje ya Tanzania οΏ½

08/07/2023

🚨 TRANSFER NEWS|| π—™π—œπ—¦π—§π—’π—‘ π— π—”π—¬π—˜π—Ÿπ—˜

✍️ Mshambuliaji hatari wa Yanga Fiston Kalala Mayele ameonesha nia ya kuendelea kusalia mitaa ya Jangwani ila kinachokwamisha ni makubaliano ya mshahara na ada ya usajili ili asaini mkataba mpya utakaomuweka Yanga mpka 2026.

Fiston Mayele amebakiza mkataba wa mwaka mmoja na Maboss wa Yanga wanahaha kumuongezea mkataba mpya Mshambuliaji huyo aliemaliza msimu akiwa Mfungaji Bora wa NBC PL pamoja na CAFCC.

Ugumu uko wapi mpaka sasa...?

Mayele ameweka wazi kuwa ili asaini mkataba mpya anahitaji mshahara wa Tsh Milioni 40 na Ada ya Usajili Tsh Milioni 300.

Yanga wao wamempa Ofa ya mkataba mpya wa miaka miwili utakaomfanya alipwe Tsh Milioni 35 na Ada ya Usajili Tsh Milioni 150.

Endapo Yanga watafikia dau analotaka Mayele atasaini muda wowote na kumfanya kuwa mchezaji anaelipwa zaidi huku thamani ya mkataba wake kwa miaka mitatu kuwa Bilioni 1.7 za kitanzania (Milioni 40Γ—Miezi 36+Milioni300)

Matumaini ya Mayele kusalia Yanga ni makubwa kutokana na uhusiano wake na Maboss wa Yanga ingawa Zamalek na Pyramids wanaonekana kuanza kuteka akili ya Mcongo huyo kutokana na mzigo mkubwa waliomuandalia.

Imeandikwa na Sospeter Ilagila.

05/07/2023

π™‚π™Šπ˜Όπ™‡ π™ˆπ˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™„π™‰π™€ & π™ˆπ™‘π™‹ π˜Όπ™ˆπ™€π™’π˜Όπ™Žπ™„π™‡π™„!!

π™Šπ™π™π™„π˜Ύπ™„π˜Όπ™‡: Klabu ya Simba imetangaza Kukamilisha Usajili wa Winga wa Kimataifa wa Cameroon πŸ‡¨πŸ‡², Leandre W***y Essomba Onana πŸ‡¨πŸ‡² k**a mchezaji huru akitokea Klabu ya Rayon Sports ya Rwanda πŸ‡·πŸ‡Ό kwa Mkataba wa Miaka miwili.

Onana mwenye umri wa Miaka 23 Msimu uliopita alifanikiwa kuwa Mchezaji bora na Mfungaji bora wa Ligi Kuu Nchini Rwanda akifunga magoli 15 na kutoa asisti 10 kwenye Michezo 20 ya Ligi hiyo.Anasifika kwa kasi, chenga na stamina akiwa na mpira huku wakimfananisha na Cristiano Ronaldo kiuchezaji.

Vyanzo vyetu vya uhakika kutoka karibu kwa Mchezaji vimeeleza kuwa Simba imemsajili nyota huyo kwa dola za kimarekani 200,000 ambazo ni zaidi ya Shilingi Milioni 495 na huku akipokea Mshahara wa shilingi milioni 19 kwa Mwezi.

05/07/2023

🚨 OFFICIAL & CONFIRMED

Yanga SC wamethibitisha kumsajili Nickon Kibabage (23) Kutoka Singida Fountain Gate kwa makataba wa Miaka miwili.

04/07/2023

🚨 D E A L D O N E 🚨

Klabu ya Azam Fc imefanikiwa kunasa saini ya Mshambuliaji hatari kutoka Senegal Alassane Diao kutoka klabu ya US Goree.

30/06/2023

🚨 ERICK JOHOLA APEWA THANK YOU

Klabu ya Yanga SC imetangaza kuachana na Mlinda Mlango wake, Erick Johola ambaye amedumu kwa misimu miwili akikitumikia kikosi cha wananchi toka aliposajiliwa akitokea Aigle Noir FC ya Burundi.

26/06/2023

YANGA SC YAPIGWA RUNGU NA FIFA

Klabu ya Yanga SC imekumbwa na adhabu ya kufungiwa kufanya usajili wa Wachezaji baada ya kushindwa kumlipa aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo Luc Eymael malipo yake ya kufutwa kazi.

Wakili wa kocha huyo wa Ubelgiji alithibitisha taarifa hiyo baada ya uamuzi huo kuwasilishwa na FIFA siku ya Jumapili.

26/06/2023

NAMBA 6 MPYA

Klabu ya Yanga SC imefikia makubaliano ya kumsajili kiungo Jonas Mkude kwa mkataba wa mwaka mmoja k**a mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Simba SC.

βœ…Ni swala la Muda kutambulishwa

26/06/2023

SIMBA SC YAWEKA BAJETI NONO

CEO wa Klabu ya Simba SC, Imani Kajula amesema Bajeti ya Klabu ya Simba SC kwa msimu wa 2023/24 ni Tsh. bilioni 24.

26/06/2023

...Coastal Union imethibitisha kuachana na Benchi lao la Ufundi...

Benchi zima limepigwa SENKYU

26/06/2023

Mpaka sasa klabu ya Simba sc imeshindwa kuafikiana na mchezaji wao Isamel Sawadogo, ambapo Sawadogo amewambia viongozi wa klabu ya Simba ili akubali kuvunja mkataba inatakuwa alipwe pesa zote ambazo ni sh. 640m, lakini viongozi walipendekeza walimlipe kidogo kidogo lakini mchezaji huyo Amekataa mpaka ikamilike ndiyo atavunja mkataba


NB:MAZUNGUMZO KATI YA SAWADOGO NA SIMBA YANAENDELEA YA KUVUNJA MKATABA

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Tabata?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Website

Address


Kyela
Tabata