13/07/2026
Nyota wa zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza Wayne Rooney wakati akichambua kikosi cha timu ya taifa ya Spain kwenye michuano ya kombe la Dunia amesema uchanga wa kikosi hicho kwa washambuliaji umefanya Nyota wa Manchester City Rodri kuwa muhimu katika kikosi hicho.
Katika uchambuzi wake Rooney amesema;
"Hii ndiyo sababu, kwangu mimi, Rodri ni mchezaji muhimu sana! Wana wachezaji wachanga wa kushambulia wenye ubunifu mkubwa, lakini mara nyingi maamuzi yao uwanjani si sahihi kila wakati." 🇪🇸🧠
"Rodri ana utulivu mkubwa wa kumiliki mpira na kuudhibiti mchezo. Ni k**a kiongozi mkuu wa timu; yupo pale akisimamia na kuongoza kila kitu. Ni mchezaji wa kuvutia sana kumtazama." 👏
13/07/2026
Ukitembelea ukurasa wa Instagram wa nyota wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Ufaransa Michael Olise utakutana na picha ambazo hazina ubora na hazionekani vizuri licha ya kukua kwa teknolojia ya picha.
Wiki chache zilizopita, Olise alifuta kila kitu kwenye ukurasa wake wa Instagram, hali iliyowaachia maswali watu wengi huku wakidai ilikuwa ni hatua ya makusudi kutokana na tetesi za kuhusishwa na Real Madrid, lakini sababu halisi ni tofauti kabisa na suala zima liko hivi. 👀
Michael Olise ana mpiga picha wake binafsi wa k**e anayefahamika k**a Florence Pernet, ambaye katika misafara ya nyota huyo wa Ufaransa daima huambatana naye ili kunasa picha za mechi kwa mtindo wa kipekee ambazo baadae Olise anazichapisha picha hizo kutoka kwa mpiga picha wake kwenye kurasa zake mitandaoni.
Wakati wa Kombe la Dunia, mamlaka za Marekani zilimnyima Florence ruhusa ya kuingia nchini, hivyo mchezaji Michael Olise akafanya uamuzi kutoweka tena picha rasmi za ubora wa 4K, bali kuendelea kutumia kazi za Florence pekee ambazo amezipiga kwenye skrini ya TV akiwa na lengo la kuheshimu kazi ya mpiga picha wake.
Sasa ukurasa wake wa Instagram wa umejaa picha za skrini (screenshot) ambazo Florence hupiga akiwa anaangalia mechi kutoka nyumbani.
Ameamua kwa makusudi kutumia picha hizo badala ya picha rasmi zenye ubora wa hali ya juu ili kuhakikisha bado anakumbuka mchango wake na anabaki kuwa sehemu ya safari yake.
✍️:
13/07/2026
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya linaendelea na juhudi za kumtafuta mwananchi anayetambulika kwa jina la Mwanaliyela Wishi, anayejulikana pia k**a Yesu, mkazi wa Kijiji cha Mapogoro kilichopo Wilaya ya Mbarali ambaye anatajwa kuhusika na tuhuma za mauaji ya mkulima Juniki Mbelembe.
Kwa mujibu wa taarifa za awali, tukio hilo linadaiwa kusababishwa na mgogoro uliodaiwa kuhusisha mifugo kuingia katika shamba la marehemu hali iliyosababisha mzozo hatimaye kuwa wa vurugu na kusababisha kifo cha mkulima huyo.
Aidha, inadaiwa kuwa baada ya tukio hilo, nyumba aliyokuwa akiishi marehemu pamoja na familia yake ilidaiwa kuchomwa moto na watu wasiojulikana.
Polisi wamewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa zitakazoweza kusaidia kumk**ata mtuhumiwa huyo ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria huku wakihimizwa kudumisha amani, kuepuka kujichukulia sheria mkononi katika hatua za utatuzi wa migogoro kwenye jamii.
13/07/2026
Wakati michuano ya Kombe la Dunia ikiendelea kiungo wa England, Jude Bellingham, ameandika historia kwa kuwa kiungo wa kwanza kabisa katika historia ya michuano hiyo kufunga mabao 6 katika michuano mmoja.
Nyota huyo wa Real Madrid ameendelea kuthibitisha ubora wake kwa kuwa mhimili muhimu wa England katika safari yao ya kufuzu hatua ya nusu fainali ya Kombe la Dunia 2026.
Mpaka sasa takwimu za Jude Bellingham – Kombe la Dunia 2026
🏟️ Mechi: 5
⚽ Mabao: 6
🎯 Asisti: 2
⭐ Mchezaji Bora wa Mechi (MOTM): 3
Ikumbukwe England imefuzu hadi Nusu Fainali
akiwa na umri wa miaka 23 pekee, Bellingham tayari anaendelea kuweka rekodi ambazo hazijawahi kufikiwa na viungo wengine katika historia ya Kombe la Dunia.
12/07/2026
Aliyewahi kuwa Golikipa wa Klabu ya Yanga SC Clause Kindoki amefariki jana Jumamosi Julai 11, 2026 kwenye ajali ya pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda ikiihusisha pia lori la mizigo.
Kwa mujibu wa meneja wa zamani wa mshambuliaji, Fiston Mayele, Nestor Mutuale, amesema Kindoki amefariki saa chache baada ya kutoka uwanjani wakati timu aliyokuwa akiitumikia ya Ligi Daraja la Kwanza ya Bustras iliyopo jijini Lubumbashi nchini DR Congo iliposhinda kwa mabao 2-1 dhidi ya Et Dauphin ya Goma.
11/07/2026
Nyota wa soka kutoka Brazil Ronaldo Nazário ametoa maoni yake nyota Kylian Mbappe na safu nzima ya ushambuliaji ya timu ya taifa ya Ufaransa katika Kombe la Dunia.
Katika maelezo yake Nazario amesema "Kylian Mbappé ni mchezaji wa kipekee anayepambana kutimiza ndoto zake. Kasi yake na uwezo wake akiwa na mpira miguuni ni jambo la kuvutia sana. Watu wengi wanaweza kukimbia kwa kasi, lakini si kwa namna Mbappé anavyocheza soka. Kwangu, hilo ni jambo la kushangaza sana."
"Pia wana Ousmane Dembélé na Désiré Doué katika safu ya ushambuliaji. Unawazuiaje wachezaji hawa wenye kasi na uwezo wa ajabu wasifunge mabao? Ukweli ni ubingwa—isipokuwa k**a wewe ni shabiki wa Argentina. Sioni timu yoyote itakayoweza kuwazuia kushinda taji. Inafurahisha sana kuitazama Ufaransa ikicheza soka, hasa ukiangalia ubora wa safu yao ya ushambuliaji. Huwezi kuchoka kuwaangalia hata kidogo." Amesema Ronaldo Nazário.
11/07/2026
Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali nchini Afrika Kusini zinaripoti kifo cha staa wa Bafana Bafana na Mamelodi Sundowns, Jayden Adams (25) ambapo mpaka hivi sasa, sababu ya kifo chake hazijatajwa.
Jayden Adams, ni miongoni mwa wachezaji walioshiriki michuano ya kombe la dunia mwaka huu nchini Marekani, Mexico na Canada.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina lake lihimidiwe🙏🏾