11/06/2026
Kagua account yako leo k**a kwenye account centre utaikuta account zaidi ya moja ziondoe tu
Kesi za kufungwa kwa account zimekuwa nyingi mno na ikileta shida account moja na nyingine zinafutwa
Hakikisha kwenye account centre umeondoa account nyingine imebaki ya instagram tu
Tarehe ya kuzaliwa uliyoandika kwenye account yako iendane na ile ambayo ipo kwenye vitambulisho vyako
09/06/2026
Hisia ndizo zinazofanya mteja anunue.
Usiuze bidhaa tu, uza hisia na matokeo yake
09/06/2026
Kuna muda unaweza kujikataa na kushindwa kuona nguvu yako sababu ya majeraha uliyonayo
Kuna umuhimu mkubwa wa kujipa nafasi ya kujisamehe na kutibu majeraha na maumivu yalipo moyoni na hii itatoa fursa kubwa ya kufanya vitu vikubwa kwa ufanisi
Hayo ni miongoni mwa mambo niliyotoka nayo kwenye event ya miaka 4 ya uponyaji na ushuhuda wa kitabu cha kovu la moyo kutoka kwa mwandishi bora Adv
Mwenyezi Mungu azidi kukubariki kwa kuwafanya wengi watabasam na kupata amani ya mioyo na mtu akikaa na wewe lazima afurahi na kucheka,hongera sana
08/06/2026
Hivi kuna mwanamke bado anaamini Kwa uzuri alionao unatosha kumpa maisha mazuri bila kupambana kujijenga kiuchumi
K**a upo toroka huko
07/06/2026
Jana nilipata nafasi ya kushiriki event hii kuazimisha miaka minne ya Kitabu cha Kovu la Moyo kilichoandikwa na Adv miaka 4 ya uponyaji na ushuhuda
Ilikuwa zaidi ya event ilikuwa safari ya kujitafakari, kujielewa na kuanza kuruhusu uponyaji wa majeraha ambayo wengi hubeba kimya kimya
Kwa hakika, tuliingia tukiwa watu fulani, lakini tulitoka tukiwa na mtazamo mpya, matumaini mapya na nguvu mpya za kuendelea
Nimekuwa nikifanya consultation na wafanyabiashara wengi wakati mwingine biashara kutokufanya vyema sababu sio soko wala bidhaa ni mtu mwenyewe kukosa utulivu akili na hisia kwa ajili ya maumivu anayoyabeba muda mrefu
Haijalishi tumepitia changamoto gani na tunapitia nini tujipe nafasi ya kuponya maumivu ili kupata utulivu wa nafsi na akili na kutimiza ndoto na mafanikio na hiki kitabu kinakupa muongozo mzuri wa kujiponya
04/06/2026
Kosa la wafanyabiashara wengi ni kuangalia matokeo ya biashara nyingine bila kuelewa mfumo uliowafikisha hapo
Machimbo yana mfumo wake,biashara yako ina mfumo wake
Ukijaribu kuendesha biashara yako kwa kanuni za biashara tofauti, unaweza kujikuta unapoteza wateja na fursa za ukuaji
Jifunze kutoka kwa wengine, lakini jenga mfumo unaofaa biashara yako
Kwa sababu biashara haikui kwa kuiga kila kitu, inakua kwa kufanya maamuzi sahihi kwa mazingira yako
K**a wao huwaoni sana online usitegemee na wewe ukitumia mfumo huo ni sahihi kwako
Kabla hujataka kuiga mfumo wa mtu fulani angalia zaidi aina ya biashara yako,aina ya wateja wako,soko lako
Umewahi kusikia mfanyabiashara akisema mbona machimbo mengine hawafanyi hivi wala hawana account online na wanauza sana nami nifanye k**a wao?
04/06/2026
Kwa wapenzi wasomaji vitabu na kupenda kujifunza hii event sio ya kukosa
Hata k**a basi hujakisoma hili kitabu hii ni fursa ya kuhudhuria na kujifunza mengi zaidi
Kwenye watu wengi kuna mengi ya kujifunza na fursa pia
Fursa na Yale tunayoyaomba mara nyingine huwa yapo kwenye mazungumzo ya watu ambao hatujuani nao
Hakikisha kukutana na event k**a hizi hubaki nyuma
Usipange kukosa na lipia mapema
Kwa taarifa zaidi wasiliana na Mariam Mbano
03/06/2026
Wafanyabiashara wengi wanafanya vitu vingi kila siku wakiamini wanafanya marketing
Lakini mwisho wa siku mauzo hayaongezeki
Sababu ni kwamba marketing sio shughuli, marketing ni matokeo
Marketing halisi hujenga uaminifu,huonyesha thamani ya bidhaa au huduma yako,humsaidia mteja kufanya maamuzi na hubadilisha umakini wa watu kuwa mauzo
Biashara yako haihitaji followers wengi pekee, inahitaji mfumo unaoweza kubadilisha watazamaji kuwa wateja
Ni jambo gani kwenye carousel hii umekuwa ukifanya ukidhani ni marketing?