Kasimpya Digital

Kasimpya Digital

Share

Ukurasa huu ni Kwa ajili Habari,Michezo na matukio mbalimbali Utapata Habari zote za Ndani na Nje ya Nchi

13/07/2026

Menyekiti wa Baraza la Wazee wa CHADEMA Kanda ya Kati, Aquilin Claud, amemtaka Katibu Mkuu wa kuunda tume kuchunguza tuhuma zinazohusu matumizı ya Fedha za wadau, akısısıtiza kuwa Kiongozi yeyote anayetuhumiwa anapaswa kujiweka pembeni kupisha Uchunguzi.

13/07/2026

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeibuka mshindi wa nafasi ya pili na kutunukiwa tuzo katika kipengele cha Banda Bora upande wa Sekta ya Miliki na Real Estate wakati wa sherehe za ufungaji wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya (Sabasaba) jijini Dar es Salaam yaliyofikia kilele chake leo Julai 13, 2026.

Tuzo hiyo imepokelewa kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Daud W. Kondoro, na Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa TBA, Bi. Amina Lumuli, ambaye amesema ushindi huo unatokana na ubunifu mkubwa uliooneshwa katika maandalizi ya banda la taasisi hiyo pamoja na namna lilivyofanikiwa kuwasilisha fursa mbalimbali za uwekezaji kwa wananchi na wadau wa maendeleo.

Akizungumza na waandishi Wa habari Bi. Lumuli ameongeza kuwa TBA imeweka mkazo katika kuonesha fursa za uwekezaji kupitia mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP), sambamba na kuelimisha wananchi kuhusu miradi ya kimkakati inayotekelezwa na wakala huo katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema miongoni mwa miradi iliyovutia wageni wengi waliotembelea banda la TBA ni pamoja na ujenzi wa nyumba za gharama nafuu, miradi ya majengo ya serikali pamoja na ukarabati na uboreshaji wa miundombinu ya michezo ikiwemo Uwanja wa Benjamin Mkapa, ambayo imeendelea kuonesha uwezo wa kitaalamu wa taasisi hiyo katika sekta ya ujenzi na usimamizi wa majengo.

Bi. Lumuli amesema tuzo hiyo ni ishara ya kuendelea kuaminiwa kwa TBA na wananchi pamoja na wadau mbalimbali kutokana na huduma bora, ubunifu wa kihandisi na uwezo wa taasisi hiyo wa kutekeleza miradi yenye tija kwa maendeleo ya Taifa na ustawi wa wananchi huku akitoa Wito Kwa wawekezaji kujitokeza kuchangamkia fursa Katika miradi ya Ubia.

Sherehe za utoaji wa tuzo na ufungaji wa maonesho hayo zimeongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, huku TBA ikiendelea kutajwa miongoni mwa taasisi za serikali zinazofanya vizuri katika utoaji wa huduma, ubunifu wa kihandisi na kuvutia wawekezaji pamoja na wananchi.

13/07/2026

Mbunge wa Jimbo la Ikungi Magharibi, Elibariki Emmanuel Kingu, amesema kauli yake kuhusu mfanyabiashara maarufu nchini Nilesh Suchack haikupaswa kutafsiriwa k**a kutetea ukiukwaji wowote wa sheria katika masuala ya biashara, kodi au taratibu za kifedha.

Akizungumza katika mahojiano maalumu, Kingu amesema alichokizungumza kilikuwa katika mtazamo wa kawaida wa uendeshaji wa biashara, hususan kuhusu wafanyabiashara kutumia huduma za benki na mikopo kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao.

Amesema endapo kuna suala lolote la kisheria linalohusu biashara, kodi au miamala ya kifedha, vyombo husika vya Serikali vina wajibu wa kufuata taratibu na kuhakikisha sheria zinafuatwa.

“Nisieleweke kwamba kauli yangu ilikuwa inataka kusimama upande wa kuzuia k**a kuna mambo mengine ya kisheria au ya kibiashara. Sikumaanisha hivyo,” amesema Kingu.

Mbunge huyo amesema hawezi kuwa mtetezi wa mtu anayekwepa kulipa kodi au anayekiuka taratibu za Serikali, akisisitiza kuwa k**a kuna madeni ya kodi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yanapaswa kulipwa kwa mujibu wa sheria.

“K**a kuna kodi za Serikali zinadaiwa zilipwe katika utaratibu wa kisheria, k**a kuna mikopo kwenye benki ilipwe. Hilo ndilo jambo la msingi,” amesema.

Vilevile Kingu amekanusha dhana kwamba kauli yake ililenga “kumclear” mtu, akisema yeye si mbunge wa kutumika kwa maslahi ya mtu binafsi na kwamba maamuzi yake yanatokana na misingi anayoamini.

Amesema msimamo wake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na maslahi ya nchi unafahamika, huku akisisitiza kuwa hasukumwi na mtu yeyote katika kutoa kauli zake.

“Mimi sinunuliki na situmiki. Mimi ni mbunge ninayejitambua na ninayejiamini. Nitasimama kwenye misingi ya kile ninachokiamini,” amesema Kingu.

Kingu amesisitiza kuwa kauli yake ililenga kuweka uelewa sahihi kuhusu mazingira ya biashara na si kuingilia taratibu za Serikali, akieleza kuwa endapo kuna jambo lolote linalohitaji uchunguzi au hatua za kisheria, vyombo husika vina wajibu wa kulifanyia kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.

13/07/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Lazaro Twange, amesema amemueleza Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, mikakati mbalimbali inayotekelezwa na shirika hilo katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, kuimarisha upatikanaji wa umeme Zanzibar pamoja na kuanzisha teknolojia mpya zitakazorahisisha huduma kwa wateja.

Twange amesema hayo leo Julai 13, 2026, baada ya Rais Dkt. Mwinyi kutembelea banda la TANESCO katika kilele cha Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo alipata fursa ya kumueleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa na shirika hilo katika kuboresha sekta ya nishati nchini.

Amesema miongoni mwa mambo aliyomueleza Rais wa Zanzibar ni utekelezaji wa mkakati wa nishati safi ya kupikia kupitia mpango wa Bill Financing unaowezesha wateja wapya na waliopo kukopeshwa majiko ya umeme na kulipa gharama zake taratibu kupitia ununuzi wa umeme. Amesema mpango huo umepata mafanikio makubwa kwa kuwa zaidi ya asilimia 90 ya wanufaika wameendelea kuurejesha kwa ufanisi, hali iliyoiwezesha TANESCO kuingia ubia na sekta binafsi katika kusambaza majiko hayo kwa wananchi wengi zaidi.

Twange amesema TANESCO pia inatekeleza mradi wenye thamani ya dola za Marekani milioni 282, huku dola milioni sita zikitengwa mahsusi kwa ajili ya kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia umeme.

Amesema katika utekelezaji wa mradi huo, TANESCO inashirikiana na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) ili kuhakikisha wananchi wa Zanzibar na Tanzania Bara wananufaika na matumizi ya nishati safi, salama na nafuu zaidi.
Kuhusu upatikanaji wa umeme Zanzibar, amesema alimfahamisha Rais Dkt. Mwinyi kuhusu mradi mkubwa wa kujenga njia mpya za kusafirisha umeme kutoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar kupitia nyaya zitakazopita chini ya bahari.

Amesema mradi huo utahusisha njia tatu za umeme zitakazounganisha Dar es Salaam na Unguja, Tanga na Pemba pamoja na Kisiju na Mafia, huku akieleza kuwa mhandisi mshauri anatarajiwa kupatikana mwezi Agosti mwaka huu na mkandarasi mwezi Januari mwakani, ambapo utekelezaji wake utachukua kati ya miezi 20 hadi 22 na kuongeza uwezo wa kupeleka umeme zaidi Zanzibar ambako mahitaji yameendelea kuongezeka kutokana na ukuaji wa sekta za utalii, viwanda na huduma za kijamii.

Aidha, Twange amesema TANESCO inaendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa kwa kuanzisha mfumo wa Smart House utakaomwezesha mteja kufuatilia matumizi ya umeme ndani ya nyumba yake kupitia simu ya mkononi, ikiwa ni pamoja na kutambua kifaa kinachotumia umeme mwingi na kukizima akiwa popote alipo duniani.

Amesema sambamba na hilo shirika linaendelea kuhamasisha matumizi ya umeme katika kupikia na usafiri kupitia kampeni ya “Pika na Uendeshe kwa Umeme”, huku likiendelea kufunga vituo vya kuchaji magari ya umeme katika maeneo mbalimbali nchini ili kuendana na uwekezaji mkubwa wa Serikali katika uzalishaji wa umeme nchini.

13/07/2026

Mwenyekiti wa K**ati ya Maridhiano na aliyewahi kuwa mwanachama wa CHADEMA, Odero Charz Odero, ametoa wito kwa Viongozi mbalimbali na wanaharakati ndani na nje ya Nchi Kurekebisha kauli zao hasa wanapokuwa wanalenga Serikali na hata kumuhusisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan

Odero amesema kauli zao ziwe zinalenga kujenga Daraja la mazungumzo na Maridhiano ili muafaka wa kitaifa upatikane

Wakati huohuo akimtolea mfano Katibu mkuu wa Chama Cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA John Mnyika amesema
anachukizwa sana na kauli zake ambazo anatoa wakati akilenga Serikali na mara nyingine Moja kwa Moja kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo msemo wake wa *"Rais haramu, Serikali haramu"*

Aidha amesema Tanzania inatakiwa kurejea katika Taifa lenye upendo na mshik**ano hasa wakati huu Taifa likielekea kwenye Maridhiano hivyo kauli na misimamo mikali haisaidii

12/07/2026

Muhandisi Mshauri wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Fales Elisha Ngeleja, amesema kuwa katika mwaka wa fedha uliopita TARURA ilitengewa shilingi bilioni 229 kwa ajili ya matengenezo ya barabara mbalimbali nchini, huku wakala huo ukiendelea kutumia mbinu na teknolojia mbalimbali zinazolenga kupunguza gharama za ujenzi na kuongeza ufanisi wa matumizi ya fedha za umma.

Ngeleja amesema TARURA imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali katika kutafuta teknolojia mbadala zinazotumia rasilimali zilizopo nchini ili kupunguza gharama za utekelezaji wa miradi na kuwezesha fedha zilizookolewa kuelekezwa katika miradi mingine ya maendeleo inayowanufaisha wananchi.

Amesema kwa sasa TARURA inaendelea na ujenzi wa barabara katika mikoa ya Pwani, Dodoma, Simiyu na Njombe kwa kutumia teknolojia ya mawe, hatua inayolenga kuokoa fedha pamoja na kutathmini uwezekano wa matumizi ya rasilimali za ndani katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu nchini.

Ngeleja amesema zaidi ya shilingi bilioni 14 zimetumika kujenga barabara katika mikoa ya Mwanza, Kigoma, Ruvuma na Mvomero kwa kutumia teknolojia hiyo ya mawe, akieleza kuwa k**a wangetumia lami nyepesi gharama zingekuwa kubwa zaidi, huku matumizi ya lami nzito yangehitaji kati ya shilingi bilioni 35 hadi 40 kutekeleza miradi hiyo.

Aidha, amesema TARURA imeendelea kujenga madaraja ya mawe pamoja na vivuko vinavyorahisisha usafiri na usafirishaji wa mazao kwa wananchi wa vijijini, hususan wakulima ambao hukumbwa na changamoto za kuvusha mazao yao kwenda masokoni wakati wa mvua. Amesema hadi sasa jumla ya vivuko 80 vimejengwa katika maeneo mbalimbali nchini, huku akibainisha kuwa tangu kuanza kwa mradi wa madaraja mwaka 2017, TARURA imejenga madaraja 515 kwa gharama ya shilingi bilioni 43, tofauti na zaidi ya shilingi bilioni 155 ambazo zingetumika k**a wangetumia nondo na zege, jambo lililosababisha kuokolewa kwa zaidi ya asilimia 72 ya gharama.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi wa Community Based Routine Maintenance (CBRM) ndani ya TARURA, Injinia Richard Nisa, amesema mradi huo ni miongoni mwa miradi ya kipaumbele ya Rais inayotekelezwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.

11/07/2026

*📌Ni kuhusu utekelezaji wa miradi vijijini*

📍Dar es Salaam

*Hayo yamebainishwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakiwa kwenye maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea jijini humo*

11/07/2026

Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Mwanga na Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa, Lembrus Mchome, amesema wanachama wa chama hicho hawataki kuona ufisadi ukitokea ndani ya chama chao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mchome amedai kuwa kuna fedha za wafanyabiashara zinazopelekwa kwa viongozi wa juu lakini hazisimamiwi ipasavyo na hazifiki kwenye shughuli za chama ngazi za chini.

Mchome amepinga vikali madai ya Katibu Mkuu John Mnyika kuwa wale wanaopigania katiba ya chama wanalipwa na CCM.

"Hilo ni uzushi na uongo mkubwa, K**a Lissu na Heche waliposema kuna fedha chafu hawakushutumiwa, kwa nini sisi sasa tunashutumiwa? Katibu Mkuu asichafue watu," amesema.

Ameongeza kuwa dalili ya mgogoro ni pamoja na kutokuwepo kwa Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ wakati wa ziara ya Makamu Mwenyekiti, jambo analosema linaonyesha uongozi umegawanyika.

Amehitimisha kwa kudai ana ushahidi wa mfanyabiashara aliyetoa shilingi milioni 256 kwa kiongozi wa chama Lubumbashi mwaka jana lakini fedha hizo hazikufika hazina ya chama.

"Tunaomba wafanyabiashara wasitishe kutoa fedha kwa sasa, Turejee kwenye uhalisia wa CHADEMA wa miaka 30, Kukosoa si dhambi, ni uhuru wa kikatiba," amesisitiza Mchome.

11/07/2026

"Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang'olewa."

Mathayo 15:13
Jiunge nasi katika ibada hii ya kipekee ya maombi, ukombozi na kufunguliwa ndani ya WRC Kivule, Matembele ya Pili, jijini Dar es Salaam.

📅 Jumapili, 12 Julai 2026
🕐 Ibada ya Kwanza: Saa 1:00 asubuhi hadi Saa 6:00 mchana
🕖 Ibada ya Pili: Kuanzia Saa 7:00 mchana

Fika ukashuhudie Mungu akitang'oa kila gugu la kiroho, kifamilia, kiuchumi na kiafya katika maisha yako huku ukipokea neema mpya kupitia Kisima cha Neema.

10/07/2026

Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) imesisitiza kuwa usalama wa abiria na mizigo ni kipaumbele chake kikuu kuanzia mwanzo hadi mwisho wa safari, kupitia matumizi ya vifaa vya kuokolea, vifaa vya kuzimia moto pamoja na mifumo ya kugundua moto na moshi katika meli zake.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Julai 10, 2026, Nahodha Msaidizi wa TASHICO, Juma Chingua, amesema kampuni hiyo imejikita kuhakikisha mizigo inalindwa dhidi ya uharibifu tangu inapopokelewa hadi inapofikishwa kwa mteja, sambamba na kuhakikisha abiria wanakuwa salama wanapokuwa safarini.

Chingua amesema usafiri wa majini ni salama na wenye uhakika mkubwa, hivyo amewakaribisha wananchi kutumia huduma za meli za TASHICO zinazotoa huduma katika maziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa pamoja na maeneo mengine yanayohudumiwa na kampuni hiyo.

Kwa upande wake, Afisa Masoko Mkuu wa TASHICO, Bi. Eugenia Punjila, amesema kampuni hiyo inaendelea kutoa huduma za usafirishaji wa abiria na mizigo ndani na nje ya nchi kupitia maziwa makuu, huku ikimiliki meli mbalimbali ikiwemo MV Umoja yenye uwezo wa kubeba tani 1,200 na ML Wimbi yenye uwezo wa kubeba tani 120 ili kuwahudumia pia wateja wenye mizigo midogo.

Punjila amesema katika Ziwa Nyasa kampuni hiyo ina meli tatu zinazofanya kazi, zikiwemo mbili za mizigo zenye uwezo wa kubeba tani 1,000 zinazotumika kusafirisha makaa ya mawe kwenda nchi jirani, huku abiria wanaosafiri kati ya Kiwira na Mbambabay wakihudumiwa na meli ya MV Mbeya II.

Naye Afisa Uhusiano wa TASHICO, Edmond Rutajama, amesema meli za kampuni hiyo zinaendelea kutoa huduma ndani na nje ya Tanzania katika maziwa makuu, huku Serikali ikiwa na mpango wa kuanzisha huduma za meli katika Bahari ya Hindi. Amesema TASHICO tayari imefanya utafiti wa aina ya meli itakayoweza kutoa huduma katika maeneo ya Tanga, Mtwara na visiwa vya jirani k**a Comoro, sambamba na kuendeleza matumizi ya meli kwa shughuli za utalii, burudani na matamasha mbalimbali.

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam