13/07/2026
Mapokezi ya kishujaa kwa Matheus Cunha!
Baada ya kurejea nyumbani kutoka kwenye Kombe la Dunia 2026 akiwa na Brazil Matheus Cunha alipokelewa kwa shangwe kubwa kwenye mji wake wa nyumbani uitwao BaΓa Formosa.
Mashabiki wengi walijitokeza kumkaribisha nyota huyo wa Brazil, wakionesha heshima na upendo mkubwa kwa mchango wake akiwa na timu ya taifa kwenye michuano hiyo.
13/07/2026
Ila Chelsea kwa kuwapiga Man U ila hizi dhambi zitawalamba sana Pauni milioni 60 kwa Mount alafu mabao 4, no asist misimu 3 ni majeraha tuπ
Mount Kwa makadirio ya kiwango cha sasa cha ubadilishaji fedha, Β£250,000 kwa wiki anapoakea takribani TSh 881,350,000 (zaidi ya milioni 881 kwa wiki).
Kwa mwezi (wiki 4) analamba takribani TSh bilioni 3.53
Kwa mwaka (wiki 52) analamba takribani TSh bilioni 45.8
Na kocha amesema asiuzwe dirisha hili ana mpango nae licha ya ofa zaidi ya tano zilizowasilishwa.
Wachezaji wa mpira wanapesa wanangu waiππ
Follow NEVES sports
13/07/2026
Cristiano Ronaldo aonekana uwanjani lakini si wa mpira wa miguu.
Baada ya kumalizika kwa kampeni ya Ureno kwenye Kombe la Dunia, CR7 ametumia muda wake wa mapumziko kwa kucheza mchezo wa padel jijini Madrid.
Aliyekuwa naye ni Javier GonzΓ‘lez Barahona, mchezaji wa kulipwa wa mchezo wa padel kutoka Hispania ambaye hushiriki mashindano ya kimataifa ya mchezo huo.
Padel ni mchezo wa raketi unaofanana na mchanganyiko wa tenisi na squash.
Huchezwa zaidi kwa jozi (2 dhidi ya 2) kwenye uwanja wenye kuta za kioo, na umekuwa ukipendwa sana na wanasoka wengi k**a sehemu ya mazoezi, burudani na kujiweka fiti wakati wa mapumziko.
13/07/2026
Wachezaji wa zamani wa England wana imani kubwa kuwa timu yao itaiondoa Argentina:
π£οΈ Joe Cole: "England itampeleka Messi mapumzikoni, nina uhakika kwa 100%. Tutaifunga Argentina na kufuzu fainali ya Kombe la Dunia. Sisi ni wepesi zaidi kuliko wao."
π£οΈ Gary Neville: "Sioni jinsi England itashindwa kufunga angalau mabao mawili dhidi ya mabeki hao wa Argentina ambao ni wazito. Sisi ni wepesi, makini zaidi, na timu yetu ina nguvu zaidi."
π£οΈ Ian Wright: "Tutaifunga Argentina. Tuchel na wachezaji wake wanaijua vizuri staili ya Messi. Tutawadhibiti uwanjani hadi mwisho."
13/07/2026
Naam kile kipindi cha kudanganyana sasa kimefika rasmi.
Mambo ya "toka sijazaliwa nilikuwa naipenda klabu hii,ni ndoto yangu tangu nikiwa tumboni kwa mama,na nisiwe mnafki nilimsumbua sana mama anizae haraka ili nikatimize ndoto yangu"
ππ
13/07/2026
Mchezaji wa zamani wa Leeds player Mike Grella ameikosoa vikali timu ya taifa ya England licha ya ushindi wao dhidi ya Norway.
π£οΈ βTatizo ni kwamba hawachezi vizuri,hakuna ubora wa mpira, transitions si nzuri, na wanaacha nafasi nyingi wazi kwenye mistari uwanjani.
"Kwa kiwango cha England, ilikuwa moja ya mechi mbaya kabisa".
Grella alisema England wanashinda licha ya kutocheza vizuri, akilinganisha hali hiyo na sawa na kumwambia mtoto asiye mzuri kuwa yeye mrembo.
13/07/2026
Picha hii ilipigwa kati ya mwaka 2007-08 hivi na huyo bwana mdogo hapo golini kwa sasa sio kipa tena anacheza nafasi nyingine tofauti kwenye moja ya top club barani Ulaya.
Je! mdau unaweza kumtambua?
13/07/2026
Nyota wa Benfica na timu ya ya taifa ya Norway Andreas Schjelderup amepost picha hii ya iliyopigwa zamani kipindi akiwa mtoto akiwa pamoja na Martin Γdegaard baada ya kufunga bao dhidi ya England kwenye Kombe la Dunia.
Kutoka kumuona Γdegaard k**a idol wake akiwa mtoto, hadi kupata assist kutoka kwake kwenye robo fainali ya Kombe la Dunia licha ya kuwa waliondoshwa.πͺβ£οΈ
13/07/2026
π΄HABARI MBAYAπ³
Mshambuliaji wa Norway Alexander SΓΈrloth, ameripotiwa kupokea vitisho vya kuuawa, ikiwemo ujumbe unaomtaka ajiue mwenyewe, kufuatia kuondolewa kwa Norway na England kwenye Kombe la Dunia.
Mashambulizi hayo ya mtandaoni yamekuja baada ya SΓΈrloth kukosa nafasi ya wazi ya kufunga na kushindwa kumpasia Erling Haaland kwenye mechi dhidi ya England, jambo lililozua hasira kwa baadhi ya mashabiki.
Sourceπ° RMC Sport
13/07/2026
Hawa wahuni wawili,Cristian Romero na Lisandro MartΓnez watacheza mechi mbili tu za Premier League, kisha wataumia na kukosa mechi 15 zinazofuata.
Lakini ni kinyume kabisa wanapocheza timu ya taifa ya Argentina. Wanakuwa hatari zaidi hata kuliko wanavyokuwa kwenye Premier League, wakifanya tackles ambazo zinaonekana k**a zinaweza kuongeza rekodi zao za majeraha, lakini mara chache sana wanaumia.
Sijui tofauti ni nini kati ya kuchezea Argentina na kucheza kwenye klabu zao. Na siyo tu kuhusu kuwa fiti, pia wanafunga magoli na kutoa assists zinazosaidia timu yao ya taifa.
Ni wachezaji tofauti kabisa wanapocheza soka la kimataifa.