Tengo online tz

Tengo online tz

Share

°KWA HABARI ZA MICHEZO °TETESI ZA MICHEZO °NA MIJADALA KUHUSU MICHEZO ° NDANI NA NJE YA TANZANIA °FOLLOW, LIKE, COMMENT, SHARE,

WE ARE THE BEST IN TOWN

06/07/2026

💢Klabu ya MC Alger ya Algeria🇩🇿 imetuma ofa $200,000 (tsh 525 milion) kwenda Singida ili kumpa Mossi Nduwumwe (22).

06/07/2026

🚨 Kwenye hili dirisha kubwa la usajili Azam FC wametenga bajeti ya Tsh 8 billion ya kuleta wachezaji wapya.

Azam FC watapitisha panga kubwa wa chezaji wa kigeni wasiopungua 7/8.

Azam FC wanataka kushindana na Simba/Yanga kikamilifu.

05/07/2026

Kipa Farouk Shikalo, anayechezea soka nchini Ethiopia, anahusishwa na uwezekano wa kujiunga na klabu ya Nairobi United FC.

Kipa huyo mwenye uzoefu, ambaye alijiunga na klabu kubwa ya Ethiopia ya St. George SC kwa mkataba wa mwaka mmoja mwezi Septemba mwaka jana, sasa anawaniwa na klabu hiyo ya Nairobi huku ikijaribu kuimarisha kikosi chake kabla ya kuanza kwa msimu mpya.

05/07/2026

🚨Kuna uwezekano mkubwa Jean Charles Ahoua akarudi kucheza Tanzania na miongoni mwa timu ambazo zimeonyesha nia ya kutaka saini yaje ni Singida black Stars, Yanga Pamba jiji.

05/07/2026

🚨Simba SC wameanza mchakato wa kumsajili 'permanent' Selemani Mwalimu. Simba wanamtaka Mwalimu msimu ujao.

Mchakato umeanza rasmi kuzungumza na Wydad. Wiki ijayo kutakuwa na mwelekeo kamili.
Cc,Hans rafael

05/07/2026

Mtanzania Baraka Majogoro amejiunga na FC Platinum ya Zimbabwe k**a mchezaji huru.

Baraka ni miongoni mwa nyota wachache wa Tanzania waliothubutu kwenda kucheza soka nje ya nchi.

Amewahi pia kucheza ligi Kuu ya Afrika Kusini kunako klabu ya Chippa United.

05/07/2026

Klabu ya Singida Black Stars haikufanya makosa kumvuta huyu kijana mwenye umri wa miaka 22 kwenye safu yao ya ulinzi Kutoka Tanga hadi kuelekea kilele cha soka la Bongo Miraji Abdallah anathibitisha kuwa mabeki wa kushoto wazawa wenye viwango vikubwa bado wapo.

K**a kuna beki wa kushoto mzawa anayejua kazi yake kimya kimya bila kelele nyingi kwenye NBC Premier League kwa sasa basi ni Miraji Abdallah 'Zambo'
Baada ya kuwasha moto akiwa na Wagosi wa Kaya Coastal Union dirisha la usajili la Januari likashuhudia mwamba huyu akitua Singida Black Stars kuongeza nguvu kwenye safu ya ulinzi na michuano ya kimataifa.

Sio beki wa kushoto wa kupitika kirahisi Ana uwezo mkubwa wa kusoma hatua za winga mpinzani na kukaba kwa akili na nguvu mara nyingi akipanda mbele krosi zake na pasi zake ndefu zina uhakika wa kufika kwa mlengwa Hatoi pasi za kubahatisha anajua wapi pa kuuweka mpira.

Ameshacheza mechi ngumu za Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF Confederation Cup) msimu huu dhidi ya timu k**a CR Belouizdad na Stellenbosch FC na ameonyesha ukomavu mkubwa

Akiwa bado kijana mdogo ana kila kitu cha kumfanya kuwa mmoja wa mabeki bora zaidi wa kushoto nchini miaka ya mbele.
Hii ndio damu changa na hazina ya baadae ya klabu yake na hata timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars

03/07/2026

KRC Genk ya Ubelgiji inaripotiwa kuwa kwenye hatua za mwisho za kumsajili kinda wa Fountain Gate FC, Juma Abushiri (Chuga Boy). 🇧🇪⚽

Fountain Gate FC wamekataa ofa kubwa kutoka Azam FC

👀 Young Africans SC walionyesha nia lakini hawakuwasilisha ofa rasmi

🔥 Genk sasa wako mbele zaidi katika kuhitimisha dili hilo la mchezaji huyo chipukizi anayezidi kung’ara.

03/07/2026

Klabu ya Singida Black Stars inathibitisha kufikia makubaliano ya kumuuza mshambuliaji wetu, Mossi Nduwumwe, kwenda klabu ya Yanga kwa ada ya uhamisho wa Dola za Kimarekani 250,000 ($250,000).

Tunapenda kumshukuru Mossi kwa mchango wake mkubwa

02/07/2026

RASMI!

Asisti 27
Mabao 107
Mechi 228

Mmoja wa Wachezaji Bora Zaidi wa PSL Aondoka Sundowns

Peter Shalulile ameagana rasmi na Mamelodi Sundowns baada ya takriban miaka sita kuitumikia klabu hiyo.

Mshambuliaji huyo raia wa Namibia mwenye umri wa miaka 32 anaondoka katika klabu hiyo kubwa ya Tshwane akiwa ameshinda mataji matano ya Betway Premiership, African Football League, Nedbank Cup, MTN8 na CAF Champions League.

Mshikiliaji wa Rekodi ya Muda Wote ya PSL: Mabao 133.

Gwiji wa PSL na Sundowns.

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Telephone

Address


Mbinga
Dar Es Salaam