Yuzzo Jr

Yuzzo Jr

Share

Asante kwa kutembelea ukurasa wetu wa habari za michezo za uhakika na makala kuhusu soka saa 24. sports

26/06/2026

Nyota wa soka wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ameibuka na ujumbe wa kugusa hisia baada ya kuchapisha video inayoonesha maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Kulelea Watoto wenye Uhitaji Maalum ‘Samatta Orphanage Center’.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, leo Juni 25, 2026 Samatta ambaye kwa sasa anakipiga katika klabu ya Le Havre AC ya Ufaransa (Ligue 1), amesema mradi huo umekaribia kukamilika na kwamba umepitia changamoto nyingi kabla ya kufikia hatua ya mwisho.

Ameandika kwamba safari ya ujenzi huo imejaa uvumilivu, mapambano na imani, lakini upendo kwa Watoto wenye uhitaji umekuwa chanzo kikuu cha nguvu ya kuendeleza mradi huo.

Akirejea mafundisho ya dini, Samatta amenukuu maandiko matakatifu akisema: “Waacheni Watoto wadogo waje kwangu” (Mathayo 19:14) na pia “Kuwafanyia mema mayatima ndiyo bora” (Qur’an 2:220), akisisitiza umuhimu wa kusaidia Watoto wenye uhitaji.

Ameongeza kuwa Kituo hicho kitatoa mazingira salama, malezi bora, upendo na fursa kwa Watoto hao kutimiza ndoto zao, akisisitiza kuwa ni mradi wa moyo wake unaolenga kurejesha kwa jamii kile alichobarikiwa nacho.

Samatta amehitimisha kwa kuwataka watu kushirikiana katika kubadilisha maisha ya Watoto na kujenga taifa lenye matumaini kwa kizazi kijacho.

26/06/2026

RASMI: Huu ndio Msimamo wa Timu ILIZOFUZU, KUONDOLEWA NA KUNAFASI YA TATU.

✅ ZILIZOFUZU (Awamu ya Pili)

Kundi A: Mexico, Afrika Kusini
Kundi B: Uswizi, Kanada
Kundi C: Brazil, Morocco
Kundi D: Marekani, Australia
Kundi E: Ujerumani, Ivory Coast
Kundi F: Uholanzi, Japan
Kundi G: -
Kundi H: Uhispania, Uruguay
Kundi I: Ufaransa, Norway
Kundi J: Argentina
Kundi K: Colombia
Kundi L: England, Ghana

🟡 TIMU 3 BORA ZILIZO NAFASI YA TATU

Uswidi
Ecuador
Bosnia na Herzegovina

❌ TIMU ZILIZOONDOLEWA

Cheki
Bahrain
Curacao
Türkiye
Ekuador
Tunisia
Yordani
Panama

26/06/2026

Manchester City wamefikia makubaliano na Nottingham Forest ya kumsajili kiungo wa England, Elliot Anderson, katika moja ya usajili mkubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa kwenye soka la Uingereza.

Ada ya usajili inatajwa kuwa Pauni Milioni 106 za awali, huku nyongeza (add-ons) zikifanya thamani ya jumla kuvuka Pauni Milioni 120, na huenda ikaweka rekodi mpya ya usajili nchini England.

Anderson mwenye umri wa miaka 23 ameruhusiwa kufanyiwa vipimo vya afya akiwa nchini Marekani, ambako yuko na timu ya taifa ya England kwenye Kombe la Dunia. Mara baada ya kukamilisha vipimo na makubaliano binafsi, anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano na Manchester City.

Kiungo huyo ameivutia City baada ya msimu bora akiwa Nottingham Forest, akicheza mechi zote za Ligi Kuu ya England, kufunga mabao manne na kutoa pasi nne za mabao. Uwezo wake wa kumiliki mpira, kuvunja mashambulizi ya wapinzani na kuanzisha mashambulizi umeifanya City imuone k**a mmoja wa viungo bora chipukizi nchini England.

Manchester City inaamini Anderson atakuwa sehemu muhimu ya kuimarisha safu yao ya kiungo, hasa kufuatia mabadiliko yanayoendelea kwenye kikosi chao.

Photos from Yuzzo Jr's post 26/06/2026

•MATOKEO YA SOKA JANA•
Alhamisi, June 25,2026

🗺WORLD CUP

🇹🇷Turkey 3-2 United States🇺🇸 (HT 2-1)
⚽️Trusty 3'(Berhalter)
⚽️Guler 10'(Yilmaz)
⚽️Kokcu 31'(Elmali)
⚽️Berhalter 49'
⚽️Ayhan 90+8'

🇯🇵Japan 1-1 Sweden🇸🇪
⚽️Maeda 56'(Doan)
⚽️Elanga 62'(Gyokeres)

🇵🇾Paraguay 0-0 Australia🇦🇺

🇹🇳Tunisia 1-3 Netherlands🇳🇱 (HT 0-2)
⚽️Shkiri 3'(OG)
⚽️Brobbey 7'(Van Dijk)
⚽️Mastouri 54'(Mejbri)
⚽️Van Hecke 62'(Reijnders)

🇪🇨Ecuador 2-1 Germany🇩🇪 (HT 2-1)
⚽️Sane 2'(Wirtz)
⚽️Angulo 9'(Vite)
⚽️Plata 77'(Rodriguez)

🇨🇼Curaçao 0-2 Ivory Coast🇨🇮
⚽️Pepe 7'(Yan Diomande)
⚽️Pepe 64'(Sangare)

🇲🇦MOROCCO - BOTOLA PRO

Berkane 2-2 FAR Rabat
Meknes 0-0 Hassania Agadir
Dcheira 2-0 Tanger
Kawkab Marrakech 2-0 FUS Rabat
Renaissance Zemamra 1-1 Olympique de Safi
Union Touarga 1-2 Difaa El Jadidi
Wydad Casablanca 0-1 Maghreb Fez
Yacoub El Mansour 2-1 Raja Casablanca


25/06/2026

Timu iliyofuzu kwa hatua ya 32.

Mechi ya 1 Imethibitishwa: 🇨🇦 Kanada dhidi ya Afrika Kusini 🇿🇦 - — 29 Juni.

🇶🇦 Kombe la Dunia la FIFA 2026 — Awamu ya Timu 32 Zitafuzu

🔥 Hadi sasa timu zilizothibitishwa:

Uwanja wa hatua ya mtoano umeanza kuimarika, huku timu kadhaa zikiwa tayari zimejihakikishia nafasi zao:

🇲🇽 Mexico (Washindi wa Kundi A)

🇺🇸 USA (Wamefuzu Kundi D)

🇩🇪 Ujerumani (Wamefuzu Kundi E)

🇦🇷 Argentina (Wamefuzu Kundi J)

🇫🇷 Ufaransa (iliyofuzu kutoka Kundi I)

🇳🇴 Norway (iliyofuzu kutoka Kundi I)

🇨🇴 Colombia (Kundi K Wamefuzu)

🇨🇭 Uswizi (Wamefuzu Kundi B)

🇨🇦 Kanada (washindi wa pili wa Kundi B)

🇿🇦 Afrika Kusini (Washindi wa pili wa Kundi A)

🇧🇷 Brazil (washindi wa Kundi C)

🇲🇦 Morocco (washindi wa pili wa Kundi C)

🇧🇦 Bosnia na Herzegovina (Best loser nafasi ya tatu)

📊 Muktadha wa sifa (hii inamaanisha nini)

Michuano hiyo ina jumla ya timu 48

-Timu 32 zitafuzu kwa Raundi ya 32

-Timu 8 bora zitakazoshika nafasi ya tatu

👉 Hiyo ina maana orodha hapo juu bado haijakamilika, na timu nyingi zitathibitishwa baada ya mechi za mwisho za makundi.

25/06/2026

Baada ya Ghana kutoka sare ya 0-0 dhidi ya England, kauli ya mganga wa Ghana iliyokuwa ikisambaa kabla ya mechi imeibuka tena na kuzua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki.

“Niliwaambia mapema, England haitashinda mechi hii.”

Kauli hiyo sasa inatajwa kwa wingi mitandaoni baada ya England kushindwa kupata ushindi waliokuwa wanauhitaji dhidi ya Black Stars. Wakati wengine wakichukulia jambo hilo k**a utani wa mashabiki wa soka, wengine wanaendelea kuhusisha matokeo hayo na utabiri wa mganga huyo.

Kwa upande wa uwanjani, Ghana ilionyesha nidhamu kubwa ya kujilinda na kufanikiwa kuondoka na pointi muhimu dhidi ya moja ya timu zilizopewa nafasi kubwa kwenye mashindano hayo.

25/06/2026

South Africa imeandika historia baada ya kuichapa South Korea kwa bao 1-0 na kufuzu kwa mara ya kwanza kabisa hatua ya 32 bora ya Kombe la Dunia 2026, mafanikio yaliyowafanya Bafana Bafana kuthibitisha msemo wa “jiwe walilolikataa waashi.”

Baada ya kukumbana na kubezwa na wengi barani Afrika kabla ya mashindano kuanza, Bafana Bafana wamejibu uwanjani kwa matokeo makubwa na safari ya kihistoria. Sasa wameungana na Mexico katika orodha ya timu zilizojihakikishia nafasi ya hatua ya mtoano na watakutana na Canada, wakionyesha kuwa walistahili kuaminiwa tangu mwanzo.

Kwa upande wa South Korea, kipigo hicho kimewaacha wakimaliza nafasi ya tatu kwenye kundi na sasa watalazimika kusubiri matokeo ya makundi mengine ili kujua k**a watafuzu k**a moja ya timu bora zilizomaliza nafasi ya tatu.

Photos from Yuzzo Jr's post 25/06/2026

Shirikisho la kimataifa la mpira wa miguu (FIFA) limemfungia mechi tano kiungo wa Qatar, Assim Madibo, kufuatia rafu iliyosababisha kiungo wa Canada, Ismaël Koné, kuvunjika mguu katika mechi ya Kundi B ya Kombe la Dunia.

Madibo alionyeshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumchezea rafu kutoka nyuma Koné katika kipindi cha pili cha mchezo ambao Canada ilishinda Qatar mabao 6-0 mjini Vancouver.

Kamati ya Nidhamu ya FIFA ilisema adhabu hiyo imetolewa kutokana na kosa la uchezaji hatari, huku ikieleza kuwa uamuzi huo bado unaweza kukatiwa rufaa.

Mchezaji huyo alivunjika mifupa ya tibia na fibula katika mguu wake wa kushoto na alifanyiwa upasuaji baada ya kuondolewa uwanjani kwa machela.

Mifupa ya Tibia na fibula ni mifupa miwili mikubwa ya sehemu ya chini ya mguu kati ya goti na kifundo cha mguu.

Tukio hilo liliwashtua wachezaji na mashabiki, na kusababisha mchezo kusimamishwa kwa muda huku wahudumu wa afya wakimhudumia Koné.

Baada ya tukio hilo, Madibo alionekana kusikitishwa na kilichotokea na baadaye alimtembelea Koné hospitalini akiwa ameambatana na Waziri wa Michezo wa Qatar, katika ishara ya uungwana na mshik**ano wa kimichezo.

Photos from Yuzzo Jr's post 25/06/2026

•MATOKEO YA SOKA JANA•
Jumatano, June 24,2026

🇹🇿TANZANIA- NBC PREMIER LEAGUE

FT: Yanga 3-0 Azam
(Bacca 41’, Depu 73’p, Pacome 81’)

FT: Mtibwa 0-3 Simba
(Rushine 9’p, Mwalimu 77’, Oura 90

FT: Singida BS 3-1 TZ Prisons
(Mossi 2’, 61’, Kennedy 23’ / Sengati 49’)

FT: TRA United 1-1 Coastal Union
(Kombo 54’p / Maabad 68’p)

FT: Dodoma Jiji 0-0 JKT Tanzania

FT: Pamba Jiji 0-2 Mbeya City
(Ambokile 18’, 76’)

FT: Fountain Gate 0-1 Mashujaa
(Hussein Mihambo 86’)

FT: KMC 2-3 Namungo
(Mwijage 36’, Mohamed 70’ / Ngoy 18’, 24’, 52’)

🗺WORLD CUP

🇿🇦South Africa 1-0 South Korea🇰🇷
⚽️Maseko 63'(Moremi)

🇨🇿Czech Republic 0-3 Mexico🇲🇽
⚽️Mateo Chavez 55'(Romo)
⚽️Quinones 61'(Sanchez)
⚽️Fidalgo 90+4'(Alvarado)

🏴󠁧󠁢󠁳󠁣󠁴󠁿Scotland 0-3 Brazil🇧🇷
⚽️Vinicius Junior 7'(Rayan)
⚽️Vinicius Junior 45+3'(Guimaraes)
⚽️Cunha 60'(Guimaraes)

🇲🇦Morocco 4-2 Haiti🇭🇹 (HT 2-2)
⚽️Bono 10'(OG)
⚽️Hakimi 39'
⚽️Isidor 43'(Duverne)
⚽️Saibari 45+1'(Hakimi)
⚽️Rahimi 78'(Riad)
⚽️Yassine 89'(Rahimi)

🇧🇦Bosnia and Herzegovina 3-1 Qatar🇶🇦 (HT 2-1)
⚽️Alajbegovic 29'(Basic)
⚽️Al-Brake 34'(OG)
⚽️Al-Haydos 42'(Edmilson Junior)
⚽️Mahmic 80'(Hadzikadunic)

🇨🇭Switzerland 2-1 Canada🇨🇦
⚽️Vargas 46'(Manzambi)
⚽️Manzambi 57'(Embolo)
⚽️Promise David 76'(Saliba)

25/06/2026

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza rasmi kuwa mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho la Benki ya CRDB (CRDB Federation Cup) msimu wa 2025/26 utachezwa Julai 4, 2026 katika Uwanja wa Gombani, Pemba.

Mchezo huo mkubwa utawakutanisha Simba SC na Azam FC kuanzia saa 11:00 jioni, huku ukiwa ndio hitimisho rasmi la mashindano ya TFF kwa msimu huu.

Simba SC ilitinga fainali baada ya kuiondoa Coastal Union kwenye hatua ya nusu fainali, wakati Azam FC ilikata tiketi ya fainali kwa kuwang'oa mabingwa watetezi Yanga SC.

Mashabiki wa soka nchini sasa wanausubiri kwa hamu mchezo huo ambao unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa wa kuwania taji la CRDB Federation Cup 2026.

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Bukoba?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Website

Address

Kibeta
Bukoba
P.O.BOX1652BUKOBA