12/07/2026
Tuzo za ligi kuu ya Rwanda zinatoka usiku wa leo,tayari Jean Claude Girumugisha,amewasili eneo la tukio.
K**a nilivyo ripoti juzi usiku,Jean Claude Girumugisha atashinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka ligi kuu Rwanda.
12/07/2026
π¨UPDATES:
Ni kweli Simba SC wameulizia upatikanaji wa mshambuliaji Ismail Mgunda 'Ba' kwa waajiri wake klab ya Mashujaa FC,
Simba wakafahamishwa kuwa bado ana mkataba nao na k**a watamuhikuhitaji basi Simba SC watalazimila kuununua mkataba uliosalia π
Mpaka sasa hakuna kiongozi wa Simba SC alirewarudia Mashujaa FCβ
Kocha Steve barker anahitaji kupata mshambuliaji mmoja mzawa β³
Abdul Sopu Deal Off β
12/07/2026
MCHEZAJI MPYA WA YANGA SC MSIMU UJAO NDIO MVP WA RWANDA ππ°
Jean Girumugisha ametangazwa kuwa mchezaji bora wa msimu ndani ya Ligi Kuu ya Rwanda msimu wa 2025-2026.
Girumugisha alikuwa na kiwango bora sana hii imempa nafasi ya kuibuka mchezaji bora wa msimu .
12/07/2026
π¨Baada ya Yao Kouassi kupona nilitegemea Israel Mwenda kuwa back-up sahihi kwenye upande wa kulia, kwasababu muda mwingi aliocheza Mwenda alifanya vizuri na kuwa moja ya RB bora msimu uliomalizika.
Ila pasipo sababu zenye mashiko anaachwa na Yanga Sc,sasa ukiangalia Mwenda amekomaa vizuri kucheza hizi timu kubwa, unakua na Mwenda back-up yake sahihi kwa wachezaji wa kizawa ni yupi?
Nasikia Yanga Sc wamemchukua yule mbavu ya kulia ya Mashujaa Fc,Gamal ila kiukweli Mwenda na Gamal unaenda na yupi?
Gamal aje Yanga Sc avumiliwe wakati ilikua rahisi kubaki na Mwenda ambaye ni uhakika wa kucheza vizuri bila presha kwenye timu.
Hiyo sababu inayomuondoa Israel Mwenda pale Yanga Sc hata sio ya kimpira Kabisa..
12/07/2026
π¨ Yanga SC wanajiandaa kufanya jaribio moja kubwa na hili sio lingine ni la kumsajili winga wa Klabu ya Azam FC Iddy Nado.
Yanga SC wanamuhitaji Iddy Nado na wanaamini wana ushawishwi mkubwa wa kumpata.
Je abakie ndani ya Azam FC ama ajiunge na Yanga SC
12/07/2026
π¨πΉπΏ πππππππππ: Simba SC wanapambana kukamilisha makubaliano ya kuongeza mkataba wa David "Duchu" Kameta, na mazungumzo yanazidi kwenda vizuri kuelekea makubaliano mapya.
Vyanzo vinasema kuwa Duchu amekuwa akiweka wazi kila wakati kwamba kipaumbele chake ni Simba SC, na pale klabu ilipomletea ofa ya kuongeza mkataba, hakuwa na nia ya kuangalia ofa kutoka klabu nyingine.
Pia, Simba SC wapo kwenye mchakato wa kusajili beki mwingine wa kulia kabla ya msimu mpya kuanza.
Ingawa Shomari Kapombe anasalia kuwa mtu anayeheshimika sana na gwiji wa kweli wa Simba, klabu hiyo inapanga mipango ya mbeleni kwa kulenga kuimarisha nafasi hiyo taratibu kwa kuleta mchezaji kijana kwa ajili ya baadae.
Mkakati upo wazi: kumbakiza Duchu k**a sehemu muhimu ya kikosi huku wakiandaa kizazi kijacho kwenye upande wa kulia wa ulinzi.
12/07/2026
|| πββοΈπββοΈ TANZIA: Golikipa wa Zamani wa Young Africans Sports Club ya Tanzania Klaus Kindoki amefariki dunia usiku wa kuamkia leo kufuatia ajali mbaya ya Gari iliyotokea Kinshasa.
RIP.
12/07/2026
π¨ TAARIFA RASMI
Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) limemfuta kazi kocha mkuu Pape Thiaw pamoja na benchi lake lote la ufundi kufuatia matokeo yasiyoridhisha ya timu ya taifa katika michuano ya Kombe la Dunia la FIFA 2026.
Uamuzi huo unafungua ukurasa mpya kwa Lions of Teranga, huku Shirikisho likitarajiwa kutangaza kocha mpya katika siku zijazo. πΈπ³β½
11/07/2026
JAYDEN ADAMS (25) Nyota wa Mamelodi Sundowns na Bafana Bafana amefariki dunia siku ya leo huku sababu za awali zikitajwa kuwa ni msongo wa mawazo hivyo kumpelekea kujiuwa baada ya kumpoteza Bibi yake wakati yupo kwenye fainali za Kombe la dunia nchini Mexico.
Jayden alikuwa Nyota anayechipukia kwa kasi kwenye soka la Afrika Kusini akiwa amecheza mechi zote za Makundi za Kombe la dunia akiwa na armband yenye jina la Bibi yake ambaye ndie alianza kufariki na ukipitia Insta story yake aliweka status masaa 22 yaliyopita.
Β© Farhan Jr
11/07/2026
Shock π
Mwamba amejiua kisa mawazo tuu π
Ila Mapenzi!!!